Thursday, November 29, 2012

BONGO ALL STARS - KAZA MOYO.mp4

Tuesday, November 27, 2012

SHARO MILIONEA AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI

Yule mkali wa sanaa ya vichekesho na bongo fleva Hussein Ramadhani Mkieti,maarufu kama Sharo milionea amefariki dunia jana majira ya saa mbili usiku katika kijiji cha Lusanga-muheza,Tanga kutokana na ajali ya gari iliyotokea akiwa njiani akielekea nyumbani kwao Muheza.
akitokea Dar ea salaam. Kamanda wa Tanga Bwana Costantine Masawe amethibitisha kutokea kwa kifo cha msanii huyo. Kamanda Masawe  amesema ajali imetokea baada ya gari dogo lenye usajili na. T478 BVR Toyota Harrier lililokuwa linaendeshwa na marehemu kuacha njia na kuingia mtaroni na kusababisha umauti huo. Mpaka sasa mwili upo hospitali teule ya muheza Tanga na mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano wiki hii.  R.I,P Sharo Milionea, we realy Gonna mic u Bro.

Monday, November 19, 2012

SNOOP DOGG ATAKA KUINUNUA CELTIC NA KUMSAJILI BECKHAM

Mkongwe na mkali wa Rap kutoka nchini Marekani, Snoop Dogg ameweka wazi nia yake ya kununua hisa ya klabu ya mpira wa miguu ya Celtic ya Uingereza. Snoop ambaye amewahi kupigwa marufuku kuingia nchini uingereza kutokana na makosa yanayohusishwa na madawa ya kulevya na matumizi ya silaha za moto, ameweka wazi kuwa ameshafanya mazungumzo na rafiki yake kiungo mkali wa LA Galaxy David Beckham ili akipige katika klabu yake pindi akikamilisha taratibu. Snoop amefikia wazo hilo baada ya kuvutiwa na kocha wa Celtic, Neil Lennon, mara baada ya kuichapa Barcelona kwenye mashindano ya klabu bingwa ulaya yanayoendelea. "Sio kitu kipya  kwa supastaa wa hiphop kuwekeza kwenye michezo,lakini ni kitu kipya kwa supastaa wa hiphop kuwekeza kwenye football" alisema Snoop kupitia 'The Scottish Daily Record'. Kwaupande wangu naona ni bonge la wazo kwa mkali huyu. All the best bro.